• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji
      • Aridhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Fedha na Baishara
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano.
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba za Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Sheria
      • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977
      • Katiba inayopendekezwa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba

MADIWANI GAIRO WAIOMBA TARURA KUWABANA WAKANDARASI WANAOKWEPA KULIPA USHURU WA HUDDUMA

Posted on: January 11th, 2022

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro, limemuomba Meneja wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini-TARURA kushirikiana na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuwabana Wakandarasi wanaopewa kandarasi za ujenzi wa mabarabara, kuhakikisha wanalipa ushuru wa huduma (service levy) ili kuiwezesha Halmashauri kukusanya mapato ya ndani kupitia chanzo hichon kwa lengo kufikia makusanyo ya shilingi 23,549,234,374 iliyojiwekea katika mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Ombi hilo limetolewa na Mwenyekiti wa Halmshauri hiyo Mhe. Rachel Nyangasi pamoja na Kaimu Mkurugunzi wa Halmashauri Bi. Susan Nyanda wakati wa kikao maalum cha Baraza la Madiwani cha Kupitia, kujadili na kupitisha Mpango na Bajeti ya TARURA Wilaya ya Gairo kwa mwaka wa Fedha 2022/2023.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha mjadala wa kikao hicho Mhe. Nyangasi alimwambia Meneja wa Tarura Saimon Masala kuwa Halmashauri inapoteza fedha nyingi za ushuru wa huduma kutokana na usimamizi mbovu kwa wakandarasi hali ambayo inachangia Wakandarasi hao kutoroka na mapato ya serikali.

“Namimi ninaungana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri kukuomba Meneja wa TARURA kusaidia katika eneo hili la kukusanya ushuru wa Huduma kwa wakandarasi wote unaowapa kazi ya ujenzi wa mabarabara ya hapa Gairo”, aliomba Mhe. Nyangasi.

Akaongeza “Ushuru huu mkiusimamia vizuri Halmashauri itaweza kukusanya vizuri lakini pia itatuwezesha Waheshimiwa Madiwani kujua kwenye Mpango wa Bajeti zetu za kila mwaka tunakusanya kiasi gani kutokana na ushuru wa huduma unaopaswa kulipwa na Wakandarasi”, alibainisha Mwneyekiti huyo.

Mhe. Nyangasi akafafanua zaidi kuwa kumekuwepo na hali ya uzembe katika kufuatilia na ukusanyaji wa ushuru wa huduma kwa wakandarasi,na kuongeza kuwa hali hiyo inawanyima wananchi kunufaika na uboreshaji wa miundo mbinu ya huduma mbalimbali za kijamii kutokana na kupotea kwa fedha ambazo zingeweza kutumika katika kuwaletea maendeleo kupitia miradi mbalimbali.

“Fedha zinazo potea ni nyingi zingeweza kuwanufaisha wananchi kupitia miradi ya maendeleo ambayo Halmashauri inapanga kutekeleza kila mwaka, lakini inashindwa kutokana na ukusanyaji hafifu wa mapatao hususani kwenye eneo hili la ushuru wa huduma za kandarasi mbalimbali za ujenzi wa miundombinu ya mabarabara”, alisistiza Mhe. Nyangasi.

Akimkaribisha Mwenyekiti kufungua Kikao hicho Maalum cha Baraza la Madiwani Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Bi. Susan Nyanda alimuomba Meneja wa TARURA kushirikiana kwa pamoja katika kusimamia ukusanyaji wa ushuru huo kwa kuweka mikakati ya pamoja ya ili kuepusha utoroshwaji wa mapato kutoka kwa wakandarasi hao.



Matangazo ya Kawaida

  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2022 SHULE ZA BWENI December 03, 2021
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALICHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI GAIRO 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO KWA WAAJIRIWA WAPYA-KARIBUNI WILAYA YA GAIRO July 01, 2021
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ACHENI KUIBUA MIGOGORO NA WATENDAJI WENU,JENGENI MAHUSIANO MAZURI

    May 21, 2022
  • WATUMISHI 3, KATI YA 4 WAREJESHWA KAZINI, 1 ASIMAMISHWA KUPISHA UCHUNGUZI

    May 20, 2022
  • WADAU WA ELIMU GAIRO WAKUSANYA SH.38 MILIONI KATIKA HARAMBEE YA KUTUNISHA MFUKO WA ELIMU

    January 14, 2022
  • MADIWANI GAIRO WAIOMBA TARURA KUWABANA WAKANDARASI WANAOKWEPA KULIPA USHURU WA HUDDUMA

    January 11, 2022
  • Tazama zote

Video

TAZAMA FILAMU YA TANZANIA THE ROYAL TOUR
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • CHANEL YETU YA YOUTUBE
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255232935454

    Simu ya Kiganjani: +255 767498981

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa